The United Republic of Tanzania

SELF Microfinance Fund

Mkopo wa Pamoja

Lengo la Mkopo

Kukidhi mahitaji ya Wajasiriamali wanaoendesha Biashara Ndogo ndogo (Micro and Small Businesses) ya mtaji wa kazi wa kila siku (Working Capital).

Walengwa.

Mjasiriamali Mmoja-mmoja anaedhaminiwa na wanakikundi wenzake.

Maelezo/Vipengele vya Mkopo

Muda wa Mkopo: Mkopo wa Kwanza miezi 3 -6. Mkopo wa Pili Mpaka miezi 12.

Ratiba ya Mrejesho

Kila wiki au mara mbili kwa wiki.

Kiwango Cha Mkopo

  1. Mkopo wa kwanza: TZS 100,000 - 500,000
  2. Mkopo wa Pili: Mpaka TZS 1,000,000
  3. Mkopo wa Tatu: Mpaka TZS 2,000,000
  4. Mkopo wa Nne: Mpaka TZS 3,000,000

Mahitaji ya Kuwasilisha Kufanya Tathmini wa Mkopo.

  1. Mkopaji atimize vigezo vya ustahili.
  2. Barua ya kumpendekeza mkopaji kutoka kamati ya mikopo ya kikundi.
  3. Historia ya mikopo iliopita (marejesho na tabia).
  4. Historia ya mzunguko wa fedha inayokidhi kufanya marejesho ya mkopo.
  5. Lazima mkopaji apitie mafunzo ya SELF MF kuhusu uzoefu/uelekeo wa mikopo (Loan Orientation Training).
  6. Afisa mikopo wa SELF MF lazima aridhike kwamba mwombaji wa mkopo anaelewa vema maelezo na masharti ya mkopo.