SELF Microfinance Fund (SELF MF) imeshiriki Maadhimisho ya Wiki ya Huduma za Fedha Kitaifa yanayofanyika katika viwanja vya Usagara, Jijini Tanga, kwa kutoa elimu ya fedha na kuhamasisha matumizi sahihi ya huduma za kifedha. Kupitia ushiriki huu, wananchi wamepata fursa ya kujifunza kuhusu mikopo, akiba, bima na huduma mbalimbali zinazotolewa na SELF MF kwa ajili ya kuimarisha maendeleo ya kiuchumi.
